AdSense

Thursday 9 April 2015

On 21:38 by Unknown in    No comments
 
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho 
 
Mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho anaamini kwamba taji la mchezaji bora duniani Ballon d'Or linafaa kuondolewa.
Mourinho anasema kuwa lengo la soka linabadilika kutoka timu za soka hadi kwa wachezaji binafsi.
''Tuanaangazia mchezo wa mchezaji mmoja, pasi alizotoa na amekimbia kilomita ngapi uwanjani.Pengine ulikimbia kilomita 11 na mimi nilikimbia kilomita tisa,lakini kilomita zangu zilikuwa muhimu kushinda zako'',alisema Mourinho.
Amesema kuwa Chelsea boss Jose Mourinho believes the Ballon d'Or should be scrapped.
Je, unadhani FIFA inafaa kulifutilia mbali taji la mchezaji bora duniani.Ingia katika mtandao wetu wa facebook katika bbcswahili uweke maoni yako.

On 21:34 by Unknown in    No comments
 
Shirikisho la mpira wa miguu duniani (FIFA) limetoa viwango vipya vya soka duniani huku Tanzania na Rwanda zikishuka kwa nchi za Afrika ya Mashariki wakati Kenya, Uganda na Burundi zikipanda viwango.
Kushuka na kupanda kwa viwango kunatokana na mechi za kirafiki za kimataifa za Fifa zilizofanyika mwezi Machi , ambazo matokeo yake ni sehemu ya kigezo.
Tanzania, baada ya kutoka droo ya 1-1 na timu ya Malawi katika moja ya mechi hizo za kirafiki, imeshuka kutoka nafasi ya 100 mpaka ya 107 huku Rwanda ikishuka nafasi 10 hadi ya 74 baada ya kupokea kichapo kutoka kwa Zambia cha magoli 2-0 mwezi Machi.
Uganda ndio nchi inayoongoza katika Afrika ya Mashariki ikipanda nafasi mbili juu na kushika nafasi ya 72 baada ya kuwafunga Nigeria 1-0.
Burundi nayo imepanda kutoka nafasi ya 126 mpaka ya 123 mbali ya kutoka droo ya 2-2 na timu ya Mauritius.
Kenya pia imepanda nafasi moja juu na sasa ipo ya 117 huku ikiwa na rekodi ya kuifunga Shelisheli 2-0 katika mechi yake ya kirafiki.
Mbali na Afrika ya Mashariki, kiujumla kumekuwa na mabadiliko makubwa katika viwango hivyo vya mwezi April.
Miongoni mwa nchi zilizopanda ni Belgium ikiwa ya tatu baada ya kupanda juu nafasi moja kufuatia ushindi wake katika michuano ya Ulaya ya EUFA.
Brazil pia ni miongoni mwa nchi zilizopanda, ikiwa ya ya 5, ikipanda nafasi 1.
Nchi 10 bora katika viwango vya fifa ni
1. Ujerumani
2. Argentina
3. Belgium
4. Colombia
5. Brazil
6. Netherlands
7. Portugal
8. Uruguay
9. Swizerland
10. Uhispania

On 21:33 by Unknown in    No comments
Shepolopolo 
 
Ni kusuka au kunyoa ambapo kitendawili cha timu gani itafuzu kucheza fainali za michezo ya Afrika kwa upande wa soka la wanawake kati ya wenyeji Twiga Stars au Shepolopolo ya Zambia kitatenguliwa pale timu hizo zitakapokwaana katika mechi ya kufuzu Ijumaa jijini Dar es Salaam.
Kuelekea katika mchezo huo, makocha wa timu zote wametambiana huku kocha mwenyeji, Rogasian Kaijage wa Twiga Stars akijivunia kuwa uwanja wa nyumbani ambapo robo tatu ya mashabiki watakuwa upande wake.
Kaijage na nahodha wake Sophia Mwasikili wamewaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani kuja kuwashangilia.
Kocha wa Shepolopolo, Albert Kachinga, akiwa nyuma ya magoli 2-4 katika mchezo wa kwanza uliochezwa mjini Lusaka, amesema amefanyia kazi makosa yaliyosababishwa kufungwa na wana matumaini ya kushinda.
Zambia pia ina nafasi endapo itaifunga Stars kwa zaidi ya idadi ya magoli yale ya awali waliofungwa nchini mwao.
Mechi inatarajiwa kuanza majira ya saa 10:30 jioni kwa saa za Afrika Mashariki, na tiketi za mchezo zitauzwa saa chache kabla ya mechi eneo la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, huku viingilio vya mchezo huo vikiwa ni shilingi za Kitanzania 5000 (wastani wa dola3 za kimarekani) kwa viti maalumu na shilingi 2000 (dola 1) kwa majukwaa yaliyobakia.
Twiga Stars 
 
Twiga Stars ambayo katika mchezo wa awali iliibuka na ushindi wa mabao 4-2, inahitaji sare ya aina yoyote ili kuweza kufuzu kwa fainali za Michezo ya Afrika zitakazofanyika nchini Congo-Brazzavile mwezi Septemba.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, ameitakia kila la kheri timu ya Taifa ya Wanawake Tanzania (Twiga Stars) wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa kwa ajili ya timu.

On 21:31 by Unknown in    No comments
 
Kocha wa Taifa Stars Mart Nooij
Licha ya kupangwa katika kundi gumu na timu za Nigeria, Misri na Chad katika michuano ya kuwania kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika 2017 nchini Gabon, kocha wa timu ya taifa ya Tanzania, Mdachi Mart Nooij amesema timu yake haiziogopi timu hizo.
Ameongeza kuwa badala yake, zitegemee pia upinzani mkali kutoka kwa Stars ambayo ana amini itakuwa imejiandaa vema kwa ajili ya mashindano hayo ambapo kushinda, kufungwa au kupata sare itakuwa ni sehemu ya matokeo.
Michuano ya Cosafa itakayofanyika nchini Afrika ya Kusini siku chache zijazo itakuwa ni sehemu ya maandalizi kwa Stars, kwa mujibu wa Nooij, ambaye anasema Stars itahitajika kutoa ushindani mkubwa.
kikosi cha Taifa stars 
 
Taifa Stars itakuwa na kibarua kigumu katika kugombea nafasi mbili kwa ajili kwenda kucheza fainali.
Stars imeshuka katika viwango vya FIFA vya mwezi April vilivyotolewa Alhamis kutoka nafasi ya 100 mpaka nafasi ya 107 na kushuka huko kuna maanisha Nooij atalazimika kufanya kazi ya ziada kupenya katika tundu la sindano.
Licha ya kushuka nafasi nne katika viwango vya FIFA, Nigeria, sasa ikiwa nafasi ya 45 ni miongoni mwa timu ngumu barani Afrika zikiwa na historia ya kufuzu kucheza kombe la Mataifa ya Afrika na hata la Dunia, sambamba na Misri, ambayo imepanda nafasi 7 katika viwango hivyo na kuwa nafasi ya 51.
Katika kundi hilo, Chad ndiyo timu iliyo chini katika viwango hivyo, ikishuka nafasi 3 na kuwa nafasi ya 151

On 21:30 by Unknown in    No comments
shambulizi Milan 
 
Jaji mmoja na wakili ni miongoni mwa watu waliouawa baada ya mshukiwa mmoja kuwafyatulia risasi ndani ya mahakama moja mjini Milan nchini Italia.
Maafisa wa idara ya mahakama wanasema kuwa mshukiwa aliyefyatua risasi ni mtu mmoja aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kutangazwa kufilisika.
Shambulizi la Milan 
 
Mshukiwa huyo aliwapiga risasi watu wawili ndani ya mahakama kabla ya kumshambulia jaji ambaye angelisikiliza kesi yake ndani ya ofisi yake.
Mtu wa nne anaaminika kufariki kutokana na mshtuko wa moyo.
Maafisa wa polisi mjini Milan baada ya shambulio la mahakamani 
 
Mshukiwa huyo alikamatwa kaskazini mwa Milan akitoroka kwa pikipiki.
Haijulikani jinsi mshukiwa huyo alivyoweza kuingia ndani ya mahakama hiyo huku akiwa na bunduki, kwa kuwa wageni wote hupitia vifaa vya kuwakagua ikiwa wana silaha.

On 21:27 by Unknown in    No comments
 
Wakimbizi wa Palestina 
 
Raia wa Palestina wanasema kuwa wamekubali kushirikiana na serikali ya Syria ili kujaribu kuwafurusha wapiganaji wa IS nje ya kambi moja ya wakimbizi viungani mwa Damascus.
Tangazo hilo hilo lilifanywa na afisa mmoja wa serikali ya Palestina huko West Bank.
Wapiganaji wa IS walitekeleza shambulizi katika kambi hiyo wiki iliopita na kuweza kuiyumbisha kanbi hiyo licha ya pingamizi kutoka kwa jeshi la Palestina.
Takriban wakimbizi elfu kumi na nane wanaishi katika kambi hiyo ambayo inakabiliwa upungufu mkubwa wa vitu muhimu.

On 21:26 by Unknown in    No comments
 
Rais Hassa Rouhani wa Iran 
 
Rais wa Iran Hassan Rouhani, ametoa wito wa kusitishwa kwa mashambulio dhidi ya wapiganaji wa Kihouthi nchini Yemen, akiyataja kama makosa makubwa.
Iran pia imepinga madai ya Saudi Arabia kuwa utawala wa Tehran unawapa wapiganaji hao wa Kihouthi ambao ni wa shia mafunzo ya Kijeshi.
Balozi wa Saudi Arabi mjini Tehran, alishutishwa kufika mbele ya wizara ya mambo ya nje ya Iran, kupokea rasmi malalamishi ya Iran.
Nchini Yemen, Ndege za kivita za muungano unaongozwa na Saudi Arabia, zimefanya mashambulio zaidi ya anga dhidi ya wapiganaji wa Houthi katika maeneo ya Kaskazini, Kusini na kati kati mwa Yemen.
Wapiganaji hao wa Houthi ambao wanapinga utawala wa rais Abd Rabbu Mansour Hadi, wamechukua uthibiti wa maeneo kadhaa nchini humo katika miezi ya hivi karibuni.
Akiongea mjini Tehran, rais Rouhani alitaja mashambulio hayo kama makosa makubwa.
Awali waziri wa mambo ya nje wa Marekani John kerry alionya Iran dhidi ya kuwaunga mkono wapiganaji hao wa Houthi.
Kerry aliyasema hayo baada ya Iran kutuma manuwari mbili za kijeshi katika eneo la Guba la Aden.

On 21:22 by Unknown in    No comments
 
Akihubiri siku ya Pasaka katika Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship lililopo Mwenge katika Jiji la Dar-Es-Salaam, Askofu Mkuu Zachary Kakobe alisema kwamba, inajulikana wazi kwamba Lowassa amekuwa anautaka Urais kwa udi na uvumba kwa miaka mingi, hata mwaka 1995 alijitosa hadharani kuuwania, sasa anapodai kwamba hivi sasa kuna makundi yanayokwenda kwake kumshawishi agombee Urais, kana kwamba yeye hataki Urais, anakuwa anamdanganya nani?


Ingawa katika mahubiri hayo ya saa mbili, Kakobe hakumtaja Lowassa kwa jina, hata hivyo Kakobe alisema, "Wako watu wengine ambao inajulikana wazi kwamba wamekuwa wakiutaka Urais kwa udi na uvumba, kwa miaka mingi, lakini hivi sasa wanasema kuna makundi ya watu yanawafuata nyumbani, kuwashawishi kugombea Urais; kama vile hawautaki Urais, hivi watu hawa wanamdanganya nani?
 
"Na wale wanaokwenda kumshawishi mtu ambaye kwa miaka mingi, anajulikana kwamba anautaka Urais, hawajui kwamba nao wanafanywa kuwa wajinga? Mtu anayejulikana kwa muda mrefu kwamba anautaka Urais, ni vema akatangaza tu moja kwa moja nia yake, bila haja ya ghiliba."

Katika mahubiri yake yenye kichwa, "UPOTOSHAJI WA UKWELI", Kakobe alieleza jinsi Gavana wa Kirumi, au liwali Pontio Pilato, alivyojiunga na Viongozi wengine kupotosha ukweli wa kufufuka kwa Yesu, na kusema kwamba wanafunzi wake waliuiba mwili wake, wakati askari walinzi walipokuwa wamelala, na kuwadanganya watu, ingawa wao wenyewe waliujua ukweli.
 
"Pilato aliwadanganya watu hao kwa muda tu, lakini hatimaye ukweli ulikuwa dhahiri, walipomwona Yesu kati yao kwa muda wa siku 40. Unaweza kuwadanganya watu kwa muda tu, lakini hatimaye ukweli hudhihirika, na kumfedhehesha yule aliyeupotosha ukweli huo", alisema.

Aliendelea kusema kuwa, hata leo kuna upotoshaji wa kweli mbalimbali za kiroho na kimwili. Baada ya kuelezea juu ya baadhi ya kweli za kiroho zilizopotoshwa, aliwageukia wanasiasa waongo, akianza kwa kutoa mfano wa Waziri wa Habari wa Iraq, wakati wa vita ya mwaka 2003, Muhammad Saeed al-Sahhaf, aliyekuwa akipotosha ukweli kuhusu jinsi Iraq ilivyokuwa inapigwa vibaya katika vita hivyo, na akaendelea kusema;
 
"Kabla sijaendelea, nifafanue kwanza juu ya watu wanaopotosha ukweli, kwa kusema kwamba eti Wachungaji hawapaswi kuwakemea wanasiasa wananapopotoka. Watu hawa hawajui Biblia. Katika MAMBO YA WALAWI 4:22-23, Biblia inasema, Mtawala akifanya dhambi, inampasa Kuhani yaani Mchungaji, kumjulisha dhambi yake."

Kakobe aliendelea kusema kwamba huu ni mwaka wa Uchaguzi, hivyo Watanzania wawe makini na wanasiasa waongo wanaofanya uongo kuwa sehemu ya siasa zao.
 
"Siasa, ni Sayansi, inaitwa POLITICAL SCIENCE, na "any kind of science only deals with facts". Wanasiasa hawana budi kuwa wakweli kwa kuwa siasa ni sayansi.
 
"Siasa siyo mchezo mchafu, bali baadhi ya wanasiasa ndiyo wachafu. Msidanganywe tena na wanasiasa ambao watakuja kwenu mwaka huu na ahadi za uongo za kuibadili miji na kuifanya kuwa kama New York, kwa miaka mitano; na wengine hawana AIBU, wanaweza hata kuwaambia wakazi wa Dodoma kwamba watawaletea meli! Hamna budi kuyachunguza kwa makini maneno yao, na kuona kama ni ya kweli."

Kuhusu Katiba, Kakobe aliwaunga mkono Maaskofu waliowapa Wakristo maelekezo ya kuikataa Katiba Pendekezwa, katika Kura ya Maoni, na kusema kwamba hiyo ndiyo kazi ya Mchungaji.
 
"Mchungaji, pia ni Mwalimu, kazi yake ni kuchunga na pia kulisha kondoo (YOHANA 21:15-17), na Biblia inafafanua juu ya kazi ya Mwalimu katika ISAYA 30:20-21, ikieleza kwamba Mwalimu anatakiwa kuwaambia anaowaongoza, "Njia ni hii ifuateni, wageukapo kwenda kulia au kushoto".
 
Aliendelea kusema, "Kumekuwa na udanganyifu au upotoshaji wa ukweli kuhusu Katiba, tangu katika hatua za mwanzo kabisa za mchakato wa Katiba, ambapo Chama kimoja cha siasa, kiliwapachika makada wake katika vikundi mbalimbali, ili kiwe na wajumbe wengi.
 
"Kwa mfano Kingunge Ngombale Mwiru aliwawakilisha waganga wa kienyeji, lakini cha ajabu, ukienda kwake hata leo, hakuna kibao kwake kinachozitambulisha kazi zake za uganga wa kienyeji, kama ilivyo kwa waganga wengine! Siyo hilo tu, kote duniani, Katiba yoyote ya nchi, lazima itokane na muafaka wa Kitaifa, ili Katiba hiyo iwe na sifa ya kusomeka katika Utangulizi wake, "SISI WANANCHI".
 
"Hapa kwetu, watawala hawakutaka kabisa muafaka katika kutengeneza Katiba yetu, lakini wanadai eti, Katiba Pendekezwa, ni bora kuliko zote Afrika! Huu ni upotoshaji wa ukweli, wa hali ya juu sana."

Aliendelea kusema kwamba, Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na Sheria ya Kura ya Maoni, hazikuzingatiwa kikamilifu katika mchakato huo uliojaa udanganyifu. 
 
"Sheria ya Kura ya Maoni, Ibara ya 5(3), inasema kwamba kungetakiwa kuwepo na elimu kwa wapiga kura, kwa siku 60, mara tu baada ya Tangazo la Katiba Pendekezwa katika Gazeti la Serikali Na. 382 lililotolewa tarehe 10.10.2014, lakini elimu hiyo iliyopaswa kutolewa na Tume ya Uchaguzi, haijafanyika hadi hivi leo! 
 
V"ilevile, Sheria ya Kura ya Maoni Ibara ya 4(3) na 4(4), inasema kwamba kungetakiwa kutangazwa katika Gazeti la Serikali, SWALI LA KURA YA MAONI, ambalo wananchi wangelijibu kwa jibu la NDIYO au HAPANA, na pia Sheria ya Kura ya Maoni Ibara ya 12(1) na 12(2) na Ibara ya 16(1) inasema kwamba, kungetakiwa kuwepo na Kamati mbili za Kura ya Maoni, Kamati moja ya NDIYO, na nyingine ya HAPANA, ambazo zingejumuisha wananchi wenye misimamo tofauti kutoka katika makundi mbalimbali katika jamii, na Kamati hizo zingepiga kampeni kwa siku 30. 
 
"Yote haya hayakuzingatiwa, lakini kinyume chake, Watawala hadi hivi leo, hawataki hata kusikia watu wakisema HAPANA kwa Kura ya Maoni, na wakati huohuo, wengine bado wanataka Kura ya Maoni ifanyike Aprili 30, pamoja na kwamba imetangazwa na Tume ya Uchaguzi, kwamba imeahirishwa!

"Wachungaji wengine wenye njaa, wanathubutu kusema kwamba eti kwa sababu kwenye Katiba Pendekezwa kuna Uhuru wa kuabudu, basi sisi Wachungaji tukae kimya, mengine hayatuhusu, hawa wana njaa kali, na upeo mdogo wa uelewa wa mambo haya.
 
"Mimi sina njaa, na ninasema kwa msisitizo, Katiba ni zaidi ya Uhuru wa kuabudu. Ilikuwa rahisi kwa Pilato kuwadanganya watu wa nyakati hizo, lakini leo ni kazi sana kuwadanganya watu wanaopata maarifa na habari juu ya yote yanayofanyika kote duniani, kwa TV, Redio, Magazeti, Intaneti na Mitandao ya kijamii. 
 
"Watu wanajua kwamba kote ulimwenguni, Katiba ya Wananchi hutokana na muafaka, na Kura ya Maoni, hufanyika baada ya Kampeni ya NDIYO na HAPANA, kama ilivyofanyika Kenya ambako waliosema NDIYO waliitwa kundi la NDIZI, na waliosema HAPANA waliitwa kundi la CHUNGWA.
 
"Waliowaambia Wakristo wapige kura ya HAPANA kwenye Kura ya Maoni, ninawapa asilimia 90, hata hivyo kwa unyenyekevu, mimi ninaomba kuhitilafiana nao, kwa kuongeza kwamba Kura ya Maoni inapaswa kususiwa kabisa, kwa sababu kushiriki katika Kura hiyo, ni kuuhalalisha udanganyifu wa Watawala hawa, na kujifedhehesha mwishoni.
 
"Tangu mwanzo, watu hawa walitumia ubabe na wizi wa kura wa dhahiri katika Bunge la Katiba, na kutangaza kura feki za NDIYO za mahujaji na wajumbe wengine ambao hawakuwepo ukumbini wakati wa kupiga kura, na pia kura za Wazanzibari feki, na hivyo kupitisha kwa lazima, Katiba Pendekezwa. 
 
"Wamedhamiria kufanya hivyohivyo hata katika Kura ya Maoni, ili kuipitisha kwa lazima Katiba yao Pendekezwa; ukizingatia kwamba, ili kutimiza kusudi hilo, wameweka sheria mbaya kwa makusudi ya kuhalalisha udanganyifu.
 
"Kwa mfano Sheria ya Kura ya Maoni Ibara ya 34(2), inahalalisha wapiga kura walioandikishwa Tanzania Bara, kwenda kupiga kupiga Kura ya Maoni, huko Zanzibar. Katika mazingira haya, Kura za HAPANA zitasaidia nini? Ni kuhalalisha tu udanganyifu wao, na kujifedhehesha.

"Mwandishi Mkuu wa Katiba Pendekezwa, yeye mwenyewe amesema anapenda aitwe JOKA LA MAKENGEZA! Niliposikia juu ya Jina lake hili, nilipigwa na butwaa! 
 
Katika Biblia, Joka ni Ibilisi au Shetani (UFUNUO 12:7-9; 20:1-2), maana yake ni kwamba Mwandishi Mkuu wa Katiba Pendekezwa, ni Joka yaani Shetani, na hivyo tunaweza kusema Katiba hiyo ni ya Kishetani, maana imetokana na Shetani ambaye ni Joka lililoko kuzimu! 
 
"Kumbe basi, siyo tu kwamba Katiba Pendekezwa imeahirishwa, ila ni kwamba Mungu ameikataa tangu siku ya kwanza ya mchakato wake!
 
"Kwa sasa tuwaze tu kujiandikisha kwa wingi katika Uandikishaji wa Wapiga Kura, kwa BVR, na kuwa tayari tu kwa Uchaguzi Mkuu, na kuisahau kabisa Kura ya Maoni."

On 21:19 by Unknown in    No comments
 
Je unataka Kuwa Mrembo na Muonekano wa Kupendeza kwa Kuongeza Hips, Makalio, Mapaja, Kurefusha Nywele, Kupunguza Unene na Kuondoa Tumbo? Basi African Beauty Products Wanakuletea Hii:
Kabla ya Kutumia Dawa na Baada ya Kutumia Dawa zetu
1.Kuongeza Hips Makalio na Mapaja 100,000/
2.Kunenepesha Miguu iwe chupa ya Bia 70,000/
3.Kuwa Mnene Mwili Mzima 80,000/
4.Kupunguza Tumbo na Nyama Uzembe 80,000/
5.Kupunguza ama Kuongeza Maziwa 60,000/
6.Kuwa Mweupe na Soft Mwili Mzima 100,000/
7.Kuondoa Chunusi na Madoa 60,000/
8.Kuondoa Michirizi na Mabaka 70,000/
9.Kupunguza Unene Mwili Mzima  80,000/
10.Kuongeza urefu na unene wa Uume 90,000/
 
Bidhaa Zetu ni Uhakika Matokeo  Ndani ya Week Moja..
Tuwasiliane kwa Simu Namba:
0756697906 ,0716805391 au 0783300397
 
Kwa watu wa Dar es Salaam Utaletewa Popote Ulipo ..Kwa Watu wa Mikoani tunatuma kwa Basi
On 21:17 by Unknown in    No comments
 
Kiongozi wa Chama cha ACT - Wazalendo, Zitto Kabwe amesema zaidi ya wabunge 50 wa vyama mbalimbali vya siasa nchini watajiunga na chama hicho kipya na kugombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu.
 
Zitto ambaye alijivua ubunge wa Kigoma Kaskazini baada ya kufukuzwa uanachama wa Chadema, amebainisha kuwa wabunge hao, wakiwamo wa CCM na Chadema, ni miongoni mwa watu wanaokichangia fedha chama hicho kilichopata usajili wa kudumu Mei, mwaka jana na kuzinduliwa mwezi uliopita.
 
Pia, amewatangazia vita wabunge wa majimbo manane ya Mkoa wa Kigoma, akijigamba kuwa ili waweze kuibuka na ushindi katika uchaguzi huo ni lazima wakubali kujiunga na ACT kwa kuwa chama hicho kimejipanga kuyabeba majimbo yote.
 
Akizungumza na Gazeti  la  Mwananchi  jijini  Dar es Salaam, Zitto alisema ACT ni chama kilichojipanga na ndiyo maana haikuwa ajabu katika mkutano wake mkuu wa hivi karibuni kuhudhuriwa na wanachama zaidi ya 400 na kufanya uzinduzi wa aina yake, huku akisisitiza kuwa chama hicho kinaungwa mkono na watu wengi.
 
“Tuna wagombea ubunge wengi wakiwamo wabunge wa sasa ambao katika Uchaguzi Mkuu Oktoba hawatagombea kupitia vyama vyao vya sasa. Wapo ambao hawatakwenda hata katika kura za maoni za vyama vyao na wameshafanya uamuzi,” alisema.
 
Huku akizungumza kwa kujiamini, Zitto alisema wabunge hao ndiyo sababu ya chama hicho kuwa na uwezo wa kujiendesha na kufafanua kuwa ACT kinawakaribisha wabunge na makada wote kutoka vyama vya Chadema na CCM.
 
“Wale ambao wanabanwa CCM na kukosa uhuru wa kuhoji jambo lolote hiki (ACT) ndicho chama chao. Wale ambao wanaamini kuwa aina za siasa tulizotaka kuzifanya ndani ya Chadema tukashindwa kuzifanya na wanadhani ni siasa muhimu zinazotakiwa, wapo na sisi,” alisema.
 
Kuhusu Kigoma
“Nahitaji majimbo yote ya Kigoma kuchukuliwa na ACT bila kukosa hata moja na hili hata Serukamba (Mbunge wa Kigoma Mjini-CCM) analijua. Mwanasiasa anayetaka kuwa mbunge Kigoma lazima aje ACT,” alisema Zitto ambaye pia alirejea kauli yake kuwa atagombea ubunge katika jimbo jingine lakini siyo Kigoma Kaskazini.
 
Kauli hiyo ya Zitto inawagusa wabunge wa sasa wa majimbo ya Kigoma ambao ni; Felix Mkosamali (Muhambwe), Moses Machali (Kasulu Mjini), Agripina Buyogela (Kasulu Vijijini) na David Kafulila (Kigoma Kusini), wote wa NCCR-Mageuzi na Peter Serukamba (Kigoma Mjini, Christopher Chiza (Buyungu) na Albert Obama (Manyovu) wa CCM.
 
Alipoulizwa iwapo wabunge hao wa majimbo ya mkoa huo ni miongoni mwa watu watakaohamia chama hicho alisema, “Sasa huo ni mtizamo wenu. Ukiwa mwanasiasa lazima uwe na msingi, nataka msingi uwe Kigoma.
 
"Tutakutana tena kwenye chumba hiki (cha mikutano) baadaye mwezi Novemba ili mnisute kwa kauli yangu na hapo itakuwa baada ya matokeo kutoka. Nahitaji kushinda kila kitu."

On 21:13 by Unknown in    No comments
 
Jose Mourinho admits he is trying to be more like Sir Alex Ferguson.
The Chelsea boss has revealed his admiration for the retired Manchester United manager.
Mourinho says that dates back to when his Porto side knocked United out of the Champions League in 2004.
Costinha’s last minute goal prompted his now infamous knee-slide at Old Trafford.
But Mourinho says Ferguson’s grace in defeat has stayed with him ever since.
Jose Mourinho and Sir Alex Ferguson
Mourinho and Ferguson have a mutual respect
“That was when I felt the two faces of such a big man,” he said in an interview with the Telegraph. “The first face was the competitor, the man that tried everything to win.
“And after that I found the man with principles, with the respect for the opponent, with the fair play – I found these two faces in that period, and that was very important for me.
“In my culture, the Portuguese and the Latin culture, we don’t have that culture of the second face.
“We are in football to win and when we don’t there is not a second face most of the time.
“But when we beat United in the Champions League I got that beautiful face of a manager which I try to have myself. I try.”
Mourinho was considered by many United fans to be the ideal successor to Ferguson when the Scot retired in 2013.
But United’s board - under the recommendation of Ferguson - opted to appoint David Moyes and hand him a six-year contract.
He lasted just nine months and was replaced by Louis van Gaal last summer, while Mourinho now looks set to lead Chelsea to the title for the first time since 2010

On 21:10 by Unknown in    No comments
 
Di Maria made a positive impact against Aston Villa

Does Di Maria return?

Ashley Young's combination with Daley Blind has been influential for United recently, and the winger's return to the side sparked The Reds' five-game Premier League winning run.
Young's crossing on Saturday, though, was erratic and however maddening Angel di Maria has performed he is a reliable assister, as he proved with the cross for Wayne Rooney's half-volley.
Di Maria not only created United's winner but injected dynamism into their attack and galvanised Rooney, poor until his spectacular strike. The derby could be a turning point for the Argentine.

Will United continue their fast starts?

Bizarrely, of the last three Old Trafford derby defeats United's best performance came in the 6-1. A result skewed by Jonny Evans' slip, his red card and defensive indiscipline in the last 10 minutes, United actually began the game brightly, with Young causing Micah Richards plenty of concern.
United have begun games brightly recently
In recent weeks, United have become more watchable thanks to their front-foot starts. They scored in the opening 10 minutes against Tottenham, the first 15 at Anfield and should have struck earlier than they did against Aston Villa.

Who starts at centre-back?

Chris Smalling's rotten luck with injuries continued as he was deprived of a start against Aston Villa to allow Marcos Rojo back into the side.
Rojo returned to the United side against Aston Villa
United's improved defensive record coincided with Phil Jones' return to the first-team, yet Smalling has shone at centre-back and must be desperate to atone for his derby red card in November.
Finally, Louis van Gaal has a positive defensive headache.

Can United end their Kompany hex?

The last time City lost to United with Vincent Kompany on the pitch came way back when Rooney executed that scarcely believable bicycle kick up at the Scoreboard End in 2011.
City boast plenty of derby bogeymen. Yaya Toure has scored four against United, Edin Dzeko five and Sergio Aguero six, however Kompany has proved to be a defensive pest who relishes his duels with Rooney, despite the No.10'slscoring prowess against City.
Kompany has led City to three successive wins at Old Trafford
This could be The Blues' greatest side's last hurrah and it is perhaps about time United belatedly dominated them.

De Gea to stop mini rot?

Indisputably United's player of the season, David de Gea has, however, been culpable for the last two goals they have conceded that have suddenly offered helpless opponents hope.
The Spaniard was at fault for Preston's opener in the February FA Cup tie, too, however De Gea has overwhelmed all and sundry with his magnificence this campaign that his errors have attracted little attention, unlike three seasons ago.
De Gea was at fault for Benteke's goal on Saturday
His mistakes have not cost United points yet, either, yet for the first time this term he is experiencing a slight wobble.


On 20:53 by Unknown in    No comments
Alves joined Barcelona in 2008
 
Manchester United continue to be linked with Barcelona right-back Dani Alves despite their interest in Southampton's Nathaniel Clyne.
Alves, 31, is out of contract in the summer whereas Clyne is 24 and has two-and-a-half years worth of Premier League experience.
Brazil full-back Alves, while an asset in attack, has often been suspect in defence and he was dropped during the World Cup in favour of City reject Maicon.
Clyne is also being monitored by Chelsea, although the relentless Branislav Ivanovic is only 31 and has shown no signs of letting up this season.
Chelsea could also hijack United's bid for Mats Hummels, although they might be late after it was claimed The Reds had agreed a deal with Borussia Dortmund earlier this year.

Monday 6 April 2015

On 05:26 by Unknown in    No comments
Lori la Mizigo lenye namba za usajili T 255 CRN na lililokuwa na Tela lenye namba za usajili T 478 BCG likiwa limefunga njia baada ya kufeli breki lilipo kuwa kwenye njia kubwa katika eneo la Mbezi Mwisho, Jijini Dar es salaam. Kwa mujibu wa Dereva wa Lori hilo aliejitambulisha kwa jina moja la Bw. Sendegwa, alisema kuwa alianza safari yake ya kutoka Mkoani Singida akiwa vizuri kabisa na alipofika maendeo ya Kibamba alihisi gari yake kupoteza upepo lakini kwa wakati huo alikuwa kwenye mwendo mdogo tayari na alianza kujarubu kutafuta namna ya kusimama lakini hakufanikiwa, na alipofika maeneo ya Mbezi aliona sehemu ya kuchepuka ambayo aliona ni salama kwa upande wake na ndipo alipoamua hivyo na huko alikutana na Gari dogo aina ya Toyota Prado lenye namba za usajili T 902 DCS ambapo alilipiga pasi ubavuni na kwenda kukita kwenye baraza la moja ya nyumba zilizokuwepo kwenye eneo hilo.
Hakuna aliejeruhiwa wala kupoteza maisha kwenye ajali hiyo. 
Lori hilo linavyoonekana baada ya kufeli breki na kuja kusimama hapo. 
 
Muonekano wa Prado hiyo baada ya kupigwa pasi na Lori hilo. 
 
Dereva wa Prado hiyo (jina kapuni) akijadiliana jambo na utingo wa Lori hilo. 
 
Mashuhuda wakiangalia namna Prado hiyo ilivyopigwa pasi. 
 
Neno la Leo lililoandikwa kwenye Lori hilo. 
 
Mashuhuda wakihadithiana namna mambo yalivyokuwa. 
 
Hapa ndipo Lori hilo lilipogota. 
 
On 05:24 by Unknown in    No comments
 
Msanii wa filamu Bongo, Fatuma Ayubu ‘Bozi’ amesema kuwa migogoro yote inayomtokea aliyewahi kuwa mwandani wake, Emmanuel Elibariki ‘Nay’ ni kutokana na laana ya kumsambazia picha zake za utupu.


Akiongea  na  mwandishi wetu, Bozi alisema tatizo kubwa lililomkuta Nay kwa mpenzi wake Siwema kumfumania na njemba ni malipo ya kupuuza penzi lake na dhambi kubwa aliyomtendea ya kusambaza picha zake za utupu alizomtumia wakati walipokuwa kwenye uhusiano.

“Nilimpenda mno Nay lakini fadhila ya penzi langu akaona anidhalilishe kwa kuanika picha zangu za utupu kwenye mitandao ya kijamii,  jambo linalonisononesha mpaka kesho, naamini yaliyomtokea ni laana yangu anayotembea nayo kwani bado sijamsamehe kwa kitendo kile cha ajabu alichonifanyia,” alisema Bozi.

On 05:23 by Unknown in    No comments
 
Matukio ya ukatili dhidi ya walemavu wa ngozi, vikongwe na watu wa makundi mengine ya kijamii nchini, yametajwa kuchangiwa kwa kiasi kikubwa na hofu na kutojiamini kwa baadhi ya watu, hivyo kujikuta wakitumia nguvu za ziada kutaka kufanikisha mambo yao, badala ya kumtegemea Mungu.
 
Hayo yamebainishwa kwenye Ibada ya Sikukuu ya Pasaka katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Azania Front na Mkuu wa kanisa hilo, Askofu Dk Alex Malasusa.
 
Alisema hofu na kukosa uhakika ni chanzo kikubwa cha dhambi jambo ambalo linawafanya watu kuingia katika matendo ya ushirikina na mauaji ya binadamu wenzao.
 
“Watu wengi wamekuwa wakishiriki ushirikina na si kwamba wanapenda ushirikina, hawapendi, lakini wamejawa na hofu na hawana uhakika na ndio chanzo cha dhambi. Kumekuwapo na matukio mengi ya ushirikina ambayo si kawaida kwa binadamu aliyeumbwa na akili akayatenda."
 
Malasusa aliongeza: “Haijalishi umesoma kiasi gani, leo hii imethibitika wasomi wengi wameingia kwenye ushirikina, haijalishi una hali gani ya kiuchumi, wafanyabiashara wengi wamejiingiza kwenye ushirikina, haijalishi unapenda ibada kiasi gani, imethibitika tunaoingia na kutoka ibadani bado tunashiriki ushirikina.
 
“Ndio maana tunasikia matendo ya kusikitisha ya binadamu kwenda kuua binadamu wenzao kama albino, vikongwe kutokana na kujawa na hofu, eti wanaamini kwa kuua albino watapata fedha au mafanikio kwenye uchaguzi, huo ni uovu na akili za kishetani. Yesu aliyefufuka ndio atakayekupa mafanikio.”
On 05:21 by Unknown in    No comments
 
Wakati wakazi wengi wa Jiji la Dar es Salaam wakiwa katika harakati za kusherehekea Sikukuu ya Pasaka, dada mmoja ambaye ni mke wa mtu yeye alijikuta akiiserebukia kwa fumanizi gesti, tena akiwa na mume wa mtu! 
 
Tukio hilo lilijiri Alhamisi Kuu maeneo Buza jijini Dar, mishale ya saa 7:00 usiku huku jamii ikiwa katika harakati za kununua hiki na kile kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka iliyoadhimishwa duniani kote jana huku leo ikiwa ni Jumatatu ya Pasaka.

 
Katika fumanizi hilo, timbwili la aina yake liliibuka baada ya mwanamke huyo mwenye mwili mkubwa, kuponyoka mikononi mwa mke aliyemnasa na kutoka nduki nje akiwa mtupu bila kujali hali hiyo.
 
Awali, ilidaiwa kuwa mume huyo wa mtu aliyefahamika kwa jina la baba Somoe, mkazi wa Kongowe (nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam) alimchepuka mke wake (mama Somoe) na kuanzisha uhusiano na mwanamke huyo.

Chanzo kikazidi kudai kwamba mkewe huyo alianza kutilia shaka mwenendo wa mumewe kutokana na kubadili tabia, hasa za kuwa beneti na simu hivyo alianza kumfuatilia kwa karibu.
 
“Katika kumfuatilia, siku moja akabaini meseji. Akamuuliza mumewe kuhusu meseji hiyo naye akawayawaya bila kuwa na majibu sahihi,”kilisema chanzo hicho.
  
Habari zaidi zilisema kuwa kutokana na ukweli kwamba, ndani ya nyumba yao, mama Somoe ndiyo kajaliwa uwezo wa kumiliki fedha, alimpa masharti mumewe kwamba achague mawili, watengane na aondoke na begi lake la nguo au atoe ushirikiano, ‘mwizi’ huyo anaswe.
 
“Mume akasema cha kufia! Akakubali kutoa ushirikiano ili mchepuko wake afumaniwe,” kilidai chanzo chetu.
  
 

On 05:20 by Unknown in    No comments
 
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima jana alihubiri akiwa katika kiti cha magurudumu na kusema hawezi kuwatupa Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa kwa kuwa ni marafiki zake wa siku nyingi. 
 
Pia askofu huyo, amewataka waumini wote wa kanisa hilo kufika katika Kituo Kikuu cha Polisi, Alhamisi ijayo siku ambayo atakwenda kukamilisha mahojiano dhidi ya tuhuma za kumtukana Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Polycarp Kardinali Pengo.
 
Akihubiri mamia ya waumini waliofika kanisani hapo kwa ajili ya ibada ya Pasaka jana, Gwajima alisema kumekuwa na uvumi kwamba kuhojiwa kwake na polisi kulitokana na kuwakaribisha wanasiasa hao kanisani kwake kwa nyakati tofauti na kuzungumza na waumini wake.
 
Alisema alifahamiana na Lowassa tangu mwaka 1996 wakati huo mbunge huyo akiwa Waziri wa Ardhi na tangu kipindi hicho amekuwa mtu wake wa karibu.
 
Alisema alifahamiana na Dk Slaa tangu mwaka 1994 kabla hajagombea nafasi ya urais kupitia Chadema na kwamba tangu wakati huo amekuwa rafiki wa familia.
 
“Hawawezi kunichagulia marafiki, hawa ni watu wangu wa karibu hata kabla hawajawa na ndoto za kugombea urais, nitaendelea kuwa nao karibu,” alisema.
 
Asimulia mahojiano
Akizungumzia mahojiano yake na polisi, Gwajima aliwaeleza waumini wake kwamba mambo mengi aliyohojiwa hayakuhusiana na suala la kumkashifu Kardinali Pengo.
 
“Polisi walinihoji mambo mengi binafsi yanayonihusu mimi na hayakuhusiana kabisa na Pengo, maswali ya Pengo yalikuwa machache sana,” alisema.
 
Hata hivyo, Gwajima alisema hana ugomvi na polisi wala Serikali kwa kuwa amekuwa akitoa ushirikiano kwa vyombo hivyo. Akitoa mfano, alisema Februari mwaka huu alipeleka barua polisi kueleza anataka kudhamini kampeni kwa ajili ya kupinga mauaji ya albino kwa kushirikiana na jeshi hilo.
 
“Niliwaeleza kwamba tungezunguka na polisi mikoa yote Tanzania na wamenijibu kwamba nipeleke ratiba ya shughuli hiyo ili tuanze,” alisema.
 
Alisema pia alidhamini mafunzo ya ulinzi shirikishi kwa vijana 400 kwa kushirikiana na polisi... “Shughuli hizi zinaonyesha kwamba sina ugomvi na polisi, bali nimekuwa rafiki kwa kushiriki katika shughuli zenye masilahi kwa Taifa.”

Viongozi wamiminika
Alisema pia hana ugomvi na Serikali na kwamba viongozi wake wamekuwa wakimiminika katika kanisa lake.
 
Aliwataja viongozi hao kuwa ni Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi na Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe.
 
Viongozi wengine, alisema ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nauye, Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee na wabunge wa Viti Maalumu, Dk Mary Mwanjelwa na Vicky Kamata wote wa CCM 
  
 “Kama ningekuwa na ugomvi na Serikali viongozi hawa wasingekuja katika kanisa langu kwa nyakati tofauti. Hii inaonyesha nilivyo na uhusiano mzuri na Serikali,” alisema.
 
Alhamisi ijayo
Askofu Gwajima amewataka waumini wake kumsindikiza katika Kituo cha Polisi siku ambayo atahojiwa kwa mara nyingine. “Nitakwenda Central Police Alhamisi saa moja asubuhi, nawaomba waumini wote mfike katika eneo hilo lakini msilete fujo wala kumtukana mtu, kuweni watulivu wakati wote nitakapokuwa nahojiwa,” alisema.
 
Askofu huyo alitakiwa kuhojiwa Alhamisi iliyopita lakini polisi waliahirisha kutokana na hali yake kutokuwa ya kuridhisha.
 
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema Jeshi la Polisi halitaruhusu mkusanyiko wa watu katika eneo hilo wakati Askofu Gwajima atakapohojiwa.
 
“Atatakiwa kufika na wakili wake na mtu mmoja ambaye ataona anafaa kuingia naye kwenye mahojiano. Kama kuna waumini wanajiandaa kukusanyika katika ofisi zetu hapa Central Polisi, wafahamu kwamba haturuhusu na wakikaidi tutachukua hatua.”
 
Ilivyokuwa kanisani
Gwajima alifika katika kanisa hilo lililopo kwenye viwanja vya Tanganyika Packers Kawe saa 5.00 asubuhi na kupokewa kwa shangwe na waumini walioanza kufika tangu saa 2.00 asubuhi.
 
Msafara wa magari matatu; Toyota Land Cruiser mbili na Hammer, yaliwasili kwenye viwanja vya kanisa hilo na kulakiwa na waumini walioyazingira kwa shangwe na vigelegele wakitaka kumwona Askofu Gwajima.

Waumini hao walikuwa na shauku ya kumwona Gwajima na walionekana wakisukumana ovyo kila mmoja akitaka kumwona.
 
Akiwa amevaa suti ya rangi ya kijivu na shati jekundu, Gwajima aliteremka katika Hammer akishikiliwa na wasaidizi wake na kukalishwa katika kiti cha magurudumu mawili kilichokuwa kikisukumwa na wasaidizi hao kuelekea kwenye jukwaa la kanisa hilo.
 
Baada ya kufika, vikundi vya kwaya viliendelea kuimba na kucheza nyimbo mbalimbali za kumtukuza Mungu.
 
Gwajima alizungumza na waumini wake kuanzia saa 5.30 hadi saa 6.45, akiwaeleza kilichotokea kuanzia siku alipofika polisi kwa mara kwanza, mahojiano hadi alipotoka hospitali.
 
Katika mahubiri yake, Gwajima alisema ataendelea kuwaonya viongozi wa Serikali na wa dini watakaokosea masuala mbalimbali.
  

 “Sitajali ni kiongozi wa aina gani amekosea nitawakemea. Rais akikosea nitamkemea. Waziri akikosea nitamkemea na viongozi wa dini wakikosea nitaendelea kuwakemea,” alisema.