AdSense

Thursday 9 April 2015

On 21:30 by Unknown in    No comments
shambulizi Milan 
 
Jaji mmoja na wakili ni miongoni mwa watu waliouawa baada ya mshukiwa mmoja kuwafyatulia risasi ndani ya mahakama moja mjini Milan nchini Italia.
Maafisa wa idara ya mahakama wanasema kuwa mshukiwa aliyefyatua risasi ni mtu mmoja aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kutangazwa kufilisika.
Shambulizi la Milan 
 
Mshukiwa huyo aliwapiga risasi watu wawili ndani ya mahakama kabla ya kumshambulia jaji ambaye angelisikiliza kesi yake ndani ya ofisi yake.
Mtu wa nne anaaminika kufariki kutokana na mshtuko wa moyo.
Maafisa wa polisi mjini Milan baada ya shambulio la mahakamani 
 
Mshukiwa huyo alikamatwa kaskazini mwa Milan akitoroka kwa pikipiki.
Haijulikani jinsi mshukiwa huyo alivyoweza kuingia ndani ya mahakama hiyo huku akiwa na bunduki, kwa kuwa wageni wote hupitia vifaa vya kuwakagua ikiwa wana silaha.

0 comments:

Post a Comment