AdSense

Showing posts with label MICHEZO. Show all posts
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts

Thursday, 9 April 2015

On 21:38 by Unknown in    No comments
 
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho 
 
Mkufunzi wa Chelsea Jose Mourinho anaamini kwamba taji la mchezaji bora duniani Ballon d'Or linafaa kuondolewa.
Mourinho anasema kuwa lengo la soka linabadilika kutoka timu za soka hadi kwa wachezaji binafsi.
''Tuanaangazia mchezo wa mchezaji mmoja, pasi alizotoa na amekimbia kilomita ngapi uwanjani.Pengine ulikimbia kilomita 11 na mimi nilikimbia kilomita tisa,lakini kilomita zangu zilikuwa muhimu kushinda zako'',alisema Mourinho.
Amesema kuwa Chelsea boss Jose Mourinho believes the Ballon d'Or should be scrapped.
Je, unadhani FIFA inafaa kulifutilia mbali taji la mchezaji bora duniani.Ingia katika mtandao wetu wa facebook katika bbcswahili uweke maoni yako.

On 21:34 by Unknown in    No comments
 
Shirikisho la mpira wa miguu duniani (FIFA) limetoa viwango vipya vya soka duniani huku Tanzania na Rwanda zikishuka kwa nchi za Afrika ya Mashariki wakati Kenya, Uganda na Burundi zikipanda viwango.
Kushuka na kupanda kwa viwango kunatokana na mechi za kirafiki za kimataifa za Fifa zilizofanyika mwezi Machi , ambazo matokeo yake ni sehemu ya kigezo.
Tanzania, baada ya kutoka droo ya 1-1 na timu ya Malawi katika moja ya mechi hizo za kirafiki, imeshuka kutoka nafasi ya 100 mpaka ya 107 huku Rwanda ikishuka nafasi 10 hadi ya 74 baada ya kupokea kichapo kutoka kwa Zambia cha magoli 2-0 mwezi Machi.
Uganda ndio nchi inayoongoza katika Afrika ya Mashariki ikipanda nafasi mbili juu na kushika nafasi ya 72 baada ya kuwafunga Nigeria 1-0.
Burundi nayo imepanda kutoka nafasi ya 126 mpaka ya 123 mbali ya kutoka droo ya 2-2 na timu ya Mauritius.
Kenya pia imepanda nafasi moja juu na sasa ipo ya 117 huku ikiwa na rekodi ya kuifunga Shelisheli 2-0 katika mechi yake ya kirafiki.
Mbali na Afrika ya Mashariki, kiujumla kumekuwa na mabadiliko makubwa katika viwango hivyo vya mwezi April.
Miongoni mwa nchi zilizopanda ni Belgium ikiwa ya tatu baada ya kupanda juu nafasi moja kufuatia ushindi wake katika michuano ya Ulaya ya EUFA.
Brazil pia ni miongoni mwa nchi zilizopanda, ikiwa ya ya 5, ikipanda nafasi 1.
Nchi 10 bora katika viwango vya fifa ni
1. Ujerumani
2. Argentina
3. Belgium
4. Colombia
5. Brazil
6. Netherlands
7. Portugal
8. Uruguay
9. Swizerland
10. Uhispania

On 21:33 by Unknown in    No comments
Shepolopolo 
 
Ni kusuka au kunyoa ambapo kitendawili cha timu gani itafuzu kucheza fainali za michezo ya Afrika kwa upande wa soka la wanawake kati ya wenyeji Twiga Stars au Shepolopolo ya Zambia kitatenguliwa pale timu hizo zitakapokwaana katika mechi ya kufuzu Ijumaa jijini Dar es Salaam.
Kuelekea katika mchezo huo, makocha wa timu zote wametambiana huku kocha mwenyeji, Rogasian Kaijage wa Twiga Stars akijivunia kuwa uwanja wa nyumbani ambapo robo tatu ya mashabiki watakuwa upande wake.
Kaijage na nahodha wake Sophia Mwasikili wamewaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani kuja kuwashangilia.
Kocha wa Shepolopolo, Albert Kachinga, akiwa nyuma ya magoli 2-4 katika mchezo wa kwanza uliochezwa mjini Lusaka, amesema amefanyia kazi makosa yaliyosababishwa kufungwa na wana matumaini ya kushinda.
Zambia pia ina nafasi endapo itaifunga Stars kwa zaidi ya idadi ya magoli yale ya awali waliofungwa nchini mwao.
Mechi inatarajiwa kuanza majira ya saa 10:30 jioni kwa saa za Afrika Mashariki, na tiketi za mchezo zitauzwa saa chache kabla ya mechi eneo la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, huku viingilio vya mchezo huo vikiwa ni shilingi za Kitanzania 5000 (wastani wa dola3 za kimarekani) kwa viti maalumu na shilingi 2000 (dola 1) kwa majukwaa yaliyobakia.
Twiga Stars 
 
Twiga Stars ambayo katika mchezo wa awali iliibuka na ushindi wa mabao 4-2, inahitaji sare ya aina yoyote ili kuweza kufuzu kwa fainali za Michezo ya Afrika zitakazofanyika nchini Congo-Brazzavile mwezi Septemba.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania (TFF), Jamal Malinzi, ameitakia kila la kheri timu ya Taifa ya Wanawake Tanzania (Twiga Stars) wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa kwa ajili ya timu.

On 21:31 by Unknown in    No comments
 
Kocha wa Taifa Stars Mart Nooij
Licha ya kupangwa katika kundi gumu na timu za Nigeria, Misri na Chad katika michuano ya kuwania kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika 2017 nchini Gabon, kocha wa timu ya taifa ya Tanzania, Mdachi Mart Nooij amesema timu yake haiziogopi timu hizo.
Ameongeza kuwa badala yake, zitegemee pia upinzani mkali kutoka kwa Stars ambayo ana amini itakuwa imejiandaa vema kwa ajili ya mashindano hayo ambapo kushinda, kufungwa au kupata sare itakuwa ni sehemu ya matokeo.
Michuano ya Cosafa itakayofanyika nchini Afrika ya Kusini siku chache zijazo itakuwa ni sehemu ya maandalizi kwa Stars, kwa mujibu wa Nooij, ambaye anasema Stars itahitajika kutoa ushindani mkubwa.
kikosi cha Taifa stars 
 
Taifa Stars itakuwa na kibarua kigumu katika kugombea nafasi mbili kwa ajili kwenda kucheza fainali.
Stars imeshuka katika viwango vya FIFA vya mwezi April vilivyotolewa Alhamis kutoka nafasi ya 100 mpaka nafasi ya 107 na kushuka huko kuna maanisha Nooij atalazimika kufanya kazi ya ziada kupenya katika tundu la sindano.
Licha ya kushuka nafasi nne katika viwango vya FIFA, Nigeria, sasa ikiwa nafasi ya 45 ni miongoni mwa timu ngumu barani Afrika zikiwa na historia ya kufuzu kucheza kombe la Mataifa ya Afrika na hata la Dunia, sambamba na Misri, ambayo imepanda nafasi 7 katika viwango hivyo na kuwa nafasi ya 51.
Katika kundi hilo, Chad ndiyo timu iliyo chini katika viwango hivyo, ikishuka nafasi 3 na kuwa nafasi ya 151

Monday, 6 April 2015

On 05:15 by Unknown in    No comments
 
Novak Djokovic ameendelea kuongeza mataji ya mchezo huo na sasa yamefikia saba.
Hatua hiyo imekuja baada ya jana kunyakua ubingwa michuano ya Miami Open kwa kumbwaga mpinzani wake Andy Murray.
Ubingwa huyo namba moja kwa ubora duniani alimbwaga mpinzani wake kwa seti 7-6 ,7-3, 4-6, 6-0.
Na baada ya mechi za jana za ligi kuu ya England leo kutakuwa na mchezo mmoja ambapo Crystal Palace watawakaribisha Manchester City.

Sunday, 5 April 2015

On 19:38 by Unknown in    No comments
 
Shirikisho la soka barani Africa CAF limethibitisha kuwa Morocco itashiriki katika mechi za kufuzu kwa dimba la Afrika mwaka 2017.
Siku ya alhamisi mahakama ya kusuluhisha mizozo ya michezo Cas ilibadilisha marufuku iliowekwa na CAF dhidi ya Morrocco ya kutoshiriki michuano ya mwaka 2017 na 2019.
Lakini siku ya ijumaa mkurugenzi wa mawasiliano wa CAF Junior Binyam aliiambia BBC kwamba kuna mikutano mingi itakayofanywa kabla ya uamuzi kufanywa.
''Tusubiri kitakachofanyika'',alisema.Droo ya mechi za kufuzu inatarajiwa kufanyika tarehe 8 mwezi Aprili.
Siku ya jumapili,Shirikisho la soka barani CAF lilitanagaza kuwa lilikubali uamuzi uliofanywa na mahakama hiyo kufuatia mkutano mkuu wa kamati ya mahakama hiyo huku ikitoa sababu zao katika mtandao.