AdSense

Monday 6 April 2015

On 05:26 by Unknown in    No comments
Lori la Mizigo lenye namba za usajili T 255 CRN na lililokuwa na Tela lenye namba za usajili T 478 BCG likiwa limefunga njia baada ya kufeli breki lilipo kuwa kwenye njia kubwa katika eneo la Mbezi Mwisho, Jijini Dar es salaam. Kwa mujibu wa Dereva wa Lori hilo aliejitambulisha kwa jina moja la Bw. Sendegwa, alisema kuwa alianza safari yake ya kutoka Mkoani Singida akiwa vizuri kabisa na alipofika maendeo ya Kibamba alihisi gari yake kupoteza upepo lakini kwa wakati huo alikuwa kwenye mwendo mdogo tayari na alianza kujarubu kutafuta namna ya kusimama lakini hakufanikiwa, na alipofika maeneo ya Mbezi aliona sehemu ya kuchepuka ambayo aliona ni salama kwa upande wake na ndipo alipoamua hivyo na huko alikutana na Gari dogo aina ya Toyota Prado lenye namba za usajili T 902 DCS ambapo alilipiga pasi ubavuni na kwenda kukita kwenye baraza la moja ya nyumba zilizokuwepo kwenye eneo hilo.
Hakuna aliejeruhiwa wala kupoteza maisha kwenye ajali hiyo. 
Lori hilo linavyoonekana baada ya kufeli breki na kuja kusimama hapo. 
 
Muonekano wa Prado hiyo baada ya kupigwa pasi na Lori hilo. 
 
Dereva wa Prado hiyo (jina kapuni) akijadiliana jambo na utingo wa Lori hilo. 
 
Mashuhuda wakiangalia namna Prado hiyo ilivyopigwa pasi. 
 
Neno la Leo lililoandikwa kwenye Lori hilo. 
 
Mashuhuda wakihadithiana namna mambo yalivyokuwa. 
 
Hapa ndipo Lori hilo lilipogota. 
 

0 comments:

Post a Comment