AdSense

Sunday 5 April 2015

On 19:34 by Unknown in    No comments
 
Ibada katika kanisa moja la Kianglikana nchini Kenya ilikatizwa ghafla baada ya tishio la ugaidi siku ya Jumapili.
Waumini walihamishwa kutoka kanisani hilo baada ya gari moja kuingia ndani ya uwanja wa kanisa kimabavu.
Kenya iko katika hali ya tahadhari baada ya mauaji ya watu wasiopungua 150 kaskazini mwa taifa taifa hilo.
Ibada hiyo ya Pasaka iligeuka na kuwa mbio za mguu niponye baada ya waumini kuarifiwa kuhusu gari hilo lisilo na nia njema.
Askofu wa kanisa hilo, Julius Kalu, amesema aliarifiwa kuhusu gari ambalo liliingizwa ndani ya uwanja wa kanisa bila hilo idhini kabla ya kusimamishwa kwenye lango kuu la kanisa lenyewe.
Askofu Kalu amesema waliokuwa ndani ya gari hilo walitoroka
Polisi waliitwa, na baada ya kulikagua gari hilo walilivuta hadi makao makuu ya polisi.
Mkuu wa polisi eneo la Mombasa Robert Kitur amesema hawakupata kitu, lakini wamelizuia gari hilo kwa uchunguzi zaidi.

0 comments:

Post a Comment