AdSense

Monday 6 April 2015

On 05:13 by Unknown in    No comments
 
Mahmoud Abbas 

Rais wa Palestina Mahmoud Abbas amekataa kukubali mamilioni ya dola ambazo ni fedha za kodi ambazo zilikuwa zimezuiliwa na Israeli.
Bwana Abbas alisema kuwa aliamua kurudisha pesa hizo kwa sababu Israeli ilikuwa imekata kiasi fulani ili kulipa kile ilichosema kuwa ni madeni kwa makampuni ya nchi yake.
Bwana Abbas alisema kuwa pesa zilizokatwa ni kama thuluthi moja ya pesa zote ambazo Israeli imekuwa ikizuia.
Amesema kuwa iwapo Israeli itakosa kulipa fedha zote hizo atapeleka kesi katika mahakama ya haki ya kimataifa ICC.

0 comments:

Post a Comment